Mambo haya utayapata Vietnam tuu...

inaelekea kama jamaa anamuuliza mkewe "hivi jana usiku uliniita jina gani vile...?"
kuna anayetaka lifti? aingie tuu...
kitoweo swafiii kwa wenzetu wa huko... kinapelekwa kupikwa, baada ya maandalizi rasmi ya awali.
maalumu kwa watoto wawili tuu...
ndio, matumizi bora ya nafasi... sio nanihii!
basi la kijiji, njiani kurudi kijijini
watoto nao hajaachwa mbali...
siku ya kuhama mambo huwa hivi... na lazima tuhame!
kukosa uwezo wa kununua helmet isiwe tabu... hata hii inafaa.
timu yetu ya kijiji ikielekea uwanjani...
mnataka haki za wanyama, sawa... hatuwatembezi tena, tunawapakia kwenye piki piki zetu.
hata kitimotoz hatukibagiu... nacho kinapata "ride"
skuli basi ya kijiji njiani kuwarudisha wasomi wetu...
ndo wameshafunga mgahawa, wanarudi home taratiiiiibu...
bei ya spea na vipuri inapanda kila mara... dawa ni kubadili injini tuu!
tupo harusini... na hao ndo maharusi wetu wakiingia ukumbini!
akitokea sokoni kuelekea kwenye mgahawa wake... kuandaa misosizzz
na hii ndio camry yetu version ya vietnam... kama hutaki wewe tuu!
hawa ni wakulima wakubwa wa mboga mboga, wakiwa njiani kusambaza huduma kwa wateja wao...
eeeh.... mgahawa mtaa huu, na jiko mtaa wa saba. ni Vietnam pekee utapata staili hizi.

Wikiendi njema.

Comments

Popular posts from this blog

FAMILIA YANGU ILIPOTEMBELEA KIJIJI CHA WATOTO YATIMA CHA FURAHA MBWENI KINACHOSIMAMIWA NA MASISTA WA KATOLIKI WA SHIRIKA LA KIMISIONARI LA BIKIRA MARIA MAMA WA YATIMA SIKU YA JUMAPILI TAREHE 17 JANUARI 2016

Rest In Peace Son of Africa, Meles Zenawi.