jihadhari na omba omba..

Natumaini kwa uwezo wa Mungu mko wazima,

Leo kwenye misa ya asubuhi kanisani Azania Front mchungaji aliyekuwa
anahubiri katufunulia siri nyingi sana za sheteni nakutupa shuhuda
mbalimbali jinsi shetani anavyofanya kazi.

Moja ya ushuhuda wake ni kisa kilichotokea hivi karibuni hapa Dar es
salaam. Napenda nikushirikishe ili uchukue hatua.

Pale salender Bridge ambapo anasimama trafiki akivuta magari, kuna mdada
alikuwa ndani ya gari lake kwenye foleni akisubiri zamu yake ya kuruhusiwa
na trafiki ifike apite. ndipo aliposogea kaka mmoja ombaomba, akasogea
kwenye gari la yule dada na kuomba msaada.

Dada huyo kwa kumhurumia akamsaidia. Alipompa pesa tu mkono wa yule dada ukaota manyoya ya paka, akachanganyikiwa alipokuwa anaendelea kushangaa trafiki akawa anaruhusu magari ya upande wake yule dada akawa hawezi kuendesha gari, ndipo trafiki akamsogelea na kuuliza kulikoni?!

Yule dada akatoa mkono wake na kumuonyesha trafiki na kumsimulia
kilichotokea na bahati nzuri yule kaka aliepewa pesa alikuwa mita chache
pembeni anamuangalia yule dada. Ikabidi trafiki aende kumuuliza yule
ombaomba kulikoni?

ndipo yule ombaomba akamwambia trafiki kuwa yule dada akimbusu tu atapona mkono utarudi kawaida.basi ikabidi yule dada atelemke aende kumbusu yule kaka, alivyombusu wakapotea wote palepale, gari ya yule dada ikabaki barabarani ndipo trafiki alipoita watu wakaanza kuisukuma ile gari na
kuiweka pembeni.

kuna dada mwingine alikuwepo leo kanisani baada ya ibada akawa
anatusimulia, yeye alikuwa nyuma ya gari ya huyo dada alishuhudia hilo
tukio anasema ni tukio la kweli kabisa ameshuhudia kwa macho yake.

Hivyo jamani nawatahadharisha ndugu zangu mlio na moyo wa huruma msipende kutoa pesa zenu hovyo sababu umekutana na maskini.
Biblia inasema maskini wapo na wataendelea kuwepo, mwombe Mungu kwanza kila unapotaka kutoa sadaka yako.
Mwenye Masikio na Asikie
Mdau Dar
 
 


Comments

Popular posts from this blog

FAMILIA YANGU ILIPOTEMBELEA KIJIJI CHA WATOTO YATIMA CHA FURAHA MBWENI KINACHOSIMAMIWA NA MASISTA WA KATOLIKI WA SHIRIKA LA KIMISIONARI LA BIKIRA MARIA MAMA WA YATIMA SIKU YA JUMAPILI TAREHE 17 JANUARI 2016

Rest In Peace Son of Africa, Meles Zenawi.