Imani potofu zinazidi kutesa, Watu hawajaelimika kumbe...


Mkazi mmoja wa Wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma, Erest Khamis (45), anashikiliwa na Polisi kwa tuhuma za kushiriki kumuua baba yake mzazi wakimtuhumu kuzuia mvua kunyesha mkoani humo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Zellothe Stephen, amesema tukio hilo limetokea jana saa 2 usiku wilayani humo ambapo mtuhumiwa huyo alimshambulia baba yake, Khamis Hussein (70), kwa kumpiga kwa madai kuwa ndiye aliyesababisha mvua isinyeshe katika mkoa huo.

Ameongeza kuwa zilikuweko taarifa za muda mrefu kuwa marehemu alikuwa akihusika katika uzuiaji wa mvua ambapo baadhi ya wanakijiji walimfuata mtoto wake huyo na kumuelezea kero hiyo. Kutokana na kitendo hicho, mtoto huyo aliamua kumpiga baba yake.

Polisi watamfikisha mahakamani mtuhumiwa baada ya taratibu kukamilika.
from: www.wavuti.com

Comments

Popular posts from this blog

FAMILIA YANGU ILIPOTEMBELEA KIJIJI CHA WATOTO YATIMA CHA FURAHA MBWENI KINACHOSIMAMIWA NA MASISTA WA KATOLIKI WA SHIRIKA LA KIMISIONARI LA BIKIRA MARIA MAMA WA YATIMA SIKU YA JUMAPILI TAREHE 17 JANUARI 2016

Rest In Peace Son of Africa, Meles Zenawi.