janet na john siku ya sherehe ya kupokea kipaimara

janet na kaka yake john wakiwa meza kuu ndani ya ukumbi wa jeshi "navy" kigamboni
baadhi ya watumishi wenzake mama janet (vale) wakipata maakuli. aliyepiga suti nyeupe hapo ni da aisha... watu walikucha kweli kweli.
hapa tunamwona da hawa naye aliyepiga kivazi cha "black" na mwenzake aliyepiga "linen" makini... ni mkucho kwa saaaanaaaa!
mh. diwani mama rweyemamu na mumewe... nao walipendeza kupita kiasi. (ila ka-kamera kalikotumwa kufanya kazi hii kaligoma kumwonyesha ipasavyo mh. diwani, tunaomba radhi kwa usumbufu huo)

tukio:

katika mlolongo mzima wa sherehe hii, janet na john waliomba kusoma risala, katika risala hizo waliwashukuru wazazi wao na kuwaomba waendelee kuwasomesha ili waje kupata maisha bora. risala ya john iliwatoa watu machozi kwa sababu asilimia kubwa pale ukumbini hawakujua kama john ni yatima. ilimlazimu mama yake mlezi (vale) kwenda kuweka msisitizo baada ya risala huku akilia, kwamba hawakuwatuma (yeye na mumewe) na wala hawakujua yaliyokuwepo kwenye risala husika. kilikuwa kipindi kigumu kwa wengi waliokuwepo ukumbini, mama yake mkubwa john (dada yake vale) naye aliipokea risala huku akilia... ilisikitisha sana. tunawaombea wazazi walezi wa john (joseph na vale) Mola awazidishie na kuwawezesha watoto hao wasome.

Comments

Popular posts from this blog

FAMILIA YANGU ILIPOTEMBELEA KIJIJI CHA WATOTO YATIMA CHA FURAHA MBWENI KINACHOSIMAMIWA NA MASISTA WA KATOLIKI WA SHIRIKA LA KIMISIONARI LA BIKIRA MARIA MAMA WA YATIMA SIKU YA JUMAPILI TAREHE 17 JANUARI 2016

Rest In Peace Son of Africa, Meles Zenawi.